Svoboda | Graniru | BBC Russia | Golosameriki | Facebook
Nenda kwa yaliyomo

Teofilo wa Antiokia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro mdogo unaomuonyesha.

Teofilo wa Antiokia (kwa Kigiriki Θεόφιλος ὁ Ἀντιοχεύς, Theofilos o Antiokheus, alifariki 183/185 BK) alikuwa askofu wa 7 wa Antiokia[1] baada ya Eros na kabla ya Masimo I[2][3].

Kutoka maandishi yake (Eusebi wa Kaisarea na Jeromu walitaja vitabu mbalimbali vya Teofilo vilivyokuwepo nyakati zao, ambavyo kati yake kimebaki kile Utetezi kwa Autolycus[4], rafiki yake msomi lakini Mpagani) tunajua kwamba alizaliwa na Wapagani katika eneo la kati ya mito Tigri na Eufrate, na kwamba aliingia Kanisa kwa kupendezwa na maadili ya Wakristo na kwa kusoma Biblia, hasa vitabu vya kinabii.[5]

Kutoka kwa mwanahistoria Eusebius wa Kaisarea tunajua juhudi zake za kutetea imani sahihi na kupinga uzushi, hasa ule wa Marcion[6][7], akichangia fasihi ya Kikristo, hoja za dini, ufafanuzi wa Biblia na utetezi wa dini kwa kutumia elimu yake pana.[8]

Maandishi yake ndiyo ya zamani kuliko yale yote tuliyonayo yanayotaja Utatu Mtakatifu.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 13 Oktoba[9].

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. Eusebius, Ecclesiastical History iv. 20; Jerome Ep. ad Algas. quaest. 6.
  2. Henry Fynes Clinton, Fasti Romani
  3. John Lightfoot, S. Ignatius, vol. ii. p. 166.
  4. Jacques Paul Migne, Patrologia Graeca, t. vi. col. 1023-1168 na toleo dogo la W. G. Humphry, Cambridge 1852. Lile la Johann Carl Theodor von Otto katika Corpus apologetarum christianorum saeculi secundi vol. ii. (Jena, 1861) ndilo lililo kamili na la kufaa zaidi sana. Tafsiri za Kiingereza: Joseph Betty (Oxford 1722), W. B. Flower (London, 1860), Marcus Dods (Clark's Ante-Nicene Library), na Robert M. Grant (Clarendon Press, 1970).
  5. Apologia ad Autolycum i. 14, ii. 24.
  6. Ecclesiastical History iv. 24.
  7. https://www.santiebeati.it/dettaglio/90478
  8. William Sanday, Studia Biblica, p. 90 describes him as "one of the precursors of that group of writers who, from Irenaeus to Cyprian, not only break the obscurity which rests on the earliest history of the Church, but alike in the East and in the West carry it to the front in literary eminence, and distance all their heathen contemporaries".
  9. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.