Svoboda | Graniru | BBC Russia | Golosameriki | Facebook
 

Tanzania yawaweka kizuizini wasaka hifadhi, UNHCR yatafuta njia ya kufikia suluhu.  

Wahamiaji na Wakimbizi
World Bank/Hendri Lombard

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi, limesema linasikitishwa sana na msururu wa ujumbe wa kusikitisha ambao limekuwa likipokea kutoka kwa kikundi cha waomba hifadhi 10 ambao hivi sasa wamewekwa kizuizini katika eneo la Mutukula, kaskazini magharibi mwa Tanzania.  

UNDP Comoros/James Stapley

Ripoti ya tabianchi ni onyo kwa sayari- Guterres

Mataifa hayajafikia popote katika kiwango kinachotakiwa kukabili ongezeko la joto duniani, imesema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo huku ikisihi serikali kuchukua hatua thabiti zaidi na za kina ili kufikia malengo ya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi ya kuhakikisha ongezeko la joto halizidi nyuzijoto 1.5 katika kipimo cha Selsiyasi ifikapo mwishoni mwa karne hii.
 

Picha: UNODC

UNODC yazindua dira ya Afrika kukabili uhalifu na madawa ya kulevya ifikapo mwaka 2030

Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili uhalifu na madawa ya kulevya, UNODC, Ghada Waly amezindua dira ya mkakati wa Afrika kwa mwaka 2030, uzinduzi uliofanyika kimtandao hii leo wakati wa mkutano wa ngazi ya juu.  

TANZBATT_8/Kapteni Tumaini Bagambo

Askari walinda amani wanawake kutoka Tanzania wawatembelea wanawake Beni, DRC

Kikundi cha walinda amani wanawake kutoka Tanzania katika kikosi cha nane kinachohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa FIB MONUSCO, nchini DRC, kimewatembelea wanawake wa kata za Matembo, Nzuma na Ngadi wilaya ya Beni. 

© UNICEF/UNI322709/Haro

UN na ECOWAS walaani machafuko baada ya kutangazwa matokeo ya awali ya uraisi Niger

Umoja wa Mataifa na jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS leo wamelaani machafuko nchini Niger kufuatia tangazo la matokeo ya awali ya duru ya pili ya uchaguzi wa rais tarehe 21 Februari.

UNICEF

COVID-19 yaongeza mahitaji ya Oksijeni, WHO na wadau wachukua hatua

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na wadau wake leo wamezindua kikosi kazi cha kuhakikisha nchi za kipato cha chini na cha kati, LMICs zinapata mitungi ya hewa ya Oksijeni ambayo mahitaji yake yameongezeka hivi sasa kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.

Vidokezo vya habari