Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi, limesema linasikitishwa sana na msururu wa ujumbe wa kusikitisha ambao limekuwa likipokea kutoka kwa kikundi cha waomba hifadhi 10 ambao hivi sasa wamewekwa kizuizini katika eneo la Mutukula, kaskazini magharibi mwa Tanzania.