Fahamu dalili za magonjwa manane ya figo

Maumivu

Chanzo cha picha, Getty Images

Kwa mujibu wa utafiti wa hivi karibuni wa Shirika la India la Nephrology, watu milioni 84 duniani kote wanaugua magonjwa mbalimbali ya figo, yaani, mtu mmoja kati ya kila watu kumi duniani ana aina fulani ya ugonjwa wa figo.

Ikumbukwe kwamba kati ya sababu kumi za vifo duniani, ugonjwa wa figo uko katika nafasi ya saba.

Moja ya sababu za kuongezeka kwa magonjwa ya figo ni kwamba magonjwa haya hayazingatiwi kuwa mabaya katika hatua za mwanzo.

Dk.Milli Mathew, ambaye ni mkuu wa Hospitali ya MGM Health Care, anasema mara nyingi umakini huoneshwa kwa ugonjwa wa figo ugonjwa huo unapofikia hatua mbaya.

Kwa hiyo, ni muhimu kuelewa magonjwa ya figo na dalili zake na kumsaidia daktari katika hatua za mwanzo za ugonjwa huo.

Lakini kabla ya kuendelea na maelezo mengine, ni nini na jinsi gani figo hufanya kazi?

Je, kazi ya figo ni nini?

Figo

Chanzo cha picha, Getty Images

Figo ni moja ya viungo muhimu vya mwili wa binadamu, ambayo kazi yake kuu ni kuondoa taka kutoka mwilini kwa njia ya mkojo.

Kwa kusudi hili, figo hutenganisha vitu kutoka kwenye damu, ambavyo ni hatari kwa mwili wa binadamu, ikiwa ni pamoja na baadhi ya madini yasiyo ya lazima, na kisha damu safi huzunguka katika mwili.

Mtindo wa maisha, lishe, tabia, matatizo ya kijeni, dawa na matatizo mengine yanayohusiana na afya yanaweza kusababisha kushindwa kufanya kazi kwa figo.

Usumbufu katika utendaji wa kawaida wa figo husababishwa na magonjwa fulani. Hatari kubwa katika suala hili ni kwamba ugonjwa huo haujatambuliwa katika hatua za mwanzo na baadhi ya dalili zake hazionekani kabisa.

Dk Milli Mathew anasema, kadiri ugonjwa unavyoendelea, dalili huonekana na unaweza kuelewa maendeleo haya kupitia uchunguzi na vipimo vya afya pekee.

Hebu sasa tuambie ni magonjwa gani ya kawaida ya figo na dalili zake.

Ugonjwa sugu wa figo

Maradhi ya figo

Chanzo cha picha, Getty Images

Aina hii ya ugonjwa wa figo hudumu kwa muda mrefu na mara nyingi huwapata watu wenye kisukari au shinikizo la damu.

Katika hatua za mwanzo za ugonjwa huu, hakuna dalili zinazoweza kuonekana, lakini jambo muhimu ni kwamba ugonjwa huu unaweza kuponywa kwa matibabu sahihi.

Dalili zake ni: kutapika, kukosa hamu ya kula, kuvimba miguu na viungo, matatizo ya kupumua, kukosa usingizi na kujisaidia haja ndogo kidogo.

Mawe ya figo

Mawe ya figo kimsingi ni madini ambayo hujilimbikiza kwenye figo na kuwa na muonekano wa mawe.

Kulingana na wataalamu wa matibabu, baada ya jiwe moja au mawili kuundwa, kwa mara ya kwanza hakuna dalili na mgonjwa hana matatizo yoyote makubwa.

Tatizo hili husababishwa na unywaji wa maji kidogo, unene kupita kiasi, lishe isiyofaa na mtindo wa maisha.

Watu wanaougua ugonjwa huu hupata shida kupata haja ndogo au kuwa na damu kwenye mkojo. Watu walioathirika wanalalamika kwa maumivu kwenye eneo la figo lenye jiwe.

Ugonjwa wa figo kutokana na kisukari

Figo

Chanzo cha picha, Getty Images

Kwa mujibu wa utafiti, kila mtu wa tatu mwenye kisukari anaugua ugonjwa wa figo na figo zao kushindwa kufanya kazi.

Ugonjwa huu ni wa kawaida zaidi kwa watu ambao hawana udhibiti wa ugonjwa wa kisukari.

Dalili zake ni pamoja na maumivu ya mguu, uchovu, kupoteza uzito, upele wa mwili, na kutapika.

Ugumu wa figo na shinikizo la damu

Mbali na ugonjwa wa kisukari, ugonjwa unaoharibu figo ni shinikizo la damu, kutokana na mishipa ya damu kwenye figo kuharibika na kazi yake ya kawaida huathirika.

Kwa sababu hii, figo haiwezi kufanya kazi yake ya kusafisha vitu visivyohitajika kutoka kwenye damu na haiwezi kuondoa madini hatari kwenye mwili kutoka kwenye damu. Kwa hivyo, vitu visivyo vya lazima hujilimbikiza kwenye mishipa ya damu na shinikizo la damu huongezeka zaidi.

Dalili ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, udhaifu, maumivu ya kichwa na shingo.

Maambukizi katika njia ya mkojo

Kipimo

Chanzo cha picha, Getty Images

ingawa maambukizi ya mfumo wa mkojo sio ugonjwa wa figo moja kwa moja, huathiri figo.

Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na bakteria na iwapo bakteria hao hawatazuiliwa na kutibiwa haraka wanaweza kufika sehemu ya juu ya njia ya mkojo na kuharibu figo.

Dalili zake ni pamoja na maumivu ya mgongo, homa, haja ndogo yenye maumivu, maumivu ya tumbo, damu kwenye mkojo, kuumwa miguu na kutapika.

Ugonjwa wa figo wa polycystic

Ugonjwa huu husababishwa na uvimbe kwenye kibofu ambao hukua kwa muda na kusababisha figo kushindwa kufanya kazi. Jeni pia inaweza kuwa sababu.

Dalili za ugonjwa huu ni maumivu katika sehemu ya juu ya tumbo, maumivu upande mmoja wa tumbo, damu kwenye mkojo au bakteria.

AJ Nephropathy

Maumivu

Chanzo cha picha, Getty Images

Ugonjwa wa figo kwa kawaida huanza utotoni na wakati wa ujana.

Dk Milli Mathew anasema, katika ugonjwa huu, kuna damu kwenye mkojo. Ugonjwa huu unaweza kutambuliwa kupitia vipimo.

Figo kushindwa kufanya kazi

Katika kushindwa, figo huacha kufanya kazi, kwa sababu mara nyingi, dalili huonekana kwa watu wenye ugonjwa huu, wakati ugonjwa huo unaendelea sana.

Kuna hatua tano za ugonjwa huu na dalili hazionekani hadi hatua ya nne.

Dalili za ugonjwa huu huonekana tu wakati figo zinaacha kufanya kazi kabisa.

Dalili zinazoonekana kwa wakati huu ni pamoja na kupoteza hamu ya kula, kutapika, udhaifu mkubwa wa kimwili, uvimbe wa sehemu za mwili na usingizi.

Imetafsiriwa na Lizzy Masinga na kuhaririwa na Seif Abdalla