Israel, Jumapili imesema Iran ilifanya mashambulizi ya makombora 320 ya kivita dhidi yake katika shambulio ambalo halijawahi kushuhudiwa, lakini ulinzi wake wa anga pamoja na Marekani na nchi nyingine zinazoiunga mkono uliyatungua kwa asilimia 99.
Msemaji wa masuala ya usalama wa taifa wa White House, John Kirby, amesema Marekani na washirika wengine wanaona yalikuwa ni mafanikio ya makubwa ya kijeshi ya Israel, katika kuzima mashambulizi ya zaidi ya ndege zisizo na rubani 300 na makombora yaliyorushwa na Iran.
Donald Trump, anaelekea mahakamani Jumatatu, akiwa ni rais wa kwanza mstaafu wa Marekani kukabiliwa na mashtaka ya uhalifu na tishio la kufungwa jela iwapo atapatikana na hatia.
Nyota wa zamani wa Ligi ya Mpira wa Marekani NFL na mcheza filamu ambaye alifutiwa mashtaka ya mauaji ya mkewe na rafiki yake wa kiume katika kesi iliyoteka Marekani na dunia amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 76.
Jeshi la anga la Ukraine limesema ulinzi wa anga wa nchi hiyo ulitungua ndege 39 kati ya 40 zisizokuwa na rubani
Takribani kilo 608 za cocaine nyingi zikiwa katika mfumo wa maji zilikamatwa katika operesheni kwenye majimbo matatu
Walinzi wa pwani wamesema walipeleka boti yao ya doria katika eneo la tukio, ambapo iliwaokoa manusura 22
Hii inafuatia makundi ya kimataifa ya misaada ya kibinadamu kulalamika kuhusu vizuizi vilivyoko huko Gaza
Wakazi wa Marekani wanajiandaa kushuhudia tukio kubwa la kupatwa kwa jua Aprili Nane.
Katika mahojiano na VOA, kampeni ya Rais Joe Biden ya kutaka kuchaguliwa tena haikutilia maanani tukio moja la rekodi ya uchangishaji fedha lililofanyika Jumamosi na kampeni ya Donald Trump.
Waziri wa fedha wa Marekani, Janet Yellen, Jumapili amemwambia Waziri Mkuu wa China, Li Qiang, kuwa uwezekano wa kufanya mazungumzo magumu umeyaweka mataifa hayo mawili yenye uchumi mkubwa sana kwenye msimamo thabiti zaidi katika kipindi cha mwaka uliopita.
Wapatanishi wa Marekani na Israel wanatarajiwa mjini Cairo mwishoni mwa juma hili kwa ajili ya msukumo mpya wa kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano katika vita ambavyo vimeendelea kwa karibu nusu mwaka.
Pandisha zaidi