Bhangi ni suala nadra la makubaliano katika Amerika iliyogawanyika kisiasa, huku ukusanyaji maoni ukionyesha kwamba asilimia 88 ya Wamarekani wanaunga mkono walau kwa kiasi fulani kuhalalisha bhangi.
Serikali ya Marekani na baraza la Kitaifa la Kulinda Nchi huko Niger (CNSP), Balozi wa Marekani nchini Niger Kathleen Fitz Gibbon na Meja Jenerali Ken Ekman, Mkurugenzi wa Mikakati, Ushirikiano na Mipango wa Kamandi ya Marekani ya Afrika, watakutana na maafisa wa baraza hilo.
Rais Joe Biedn ametia saini Jumatano mswada ambao utaweza kupiga marufuku app maarufu ya TikTok kutumika kote nchini, hivyo kuongeza kitisho dhidi ya biashara za kampuni hiyo Marekani.
Maandamano ya wanaounga mkono Wapalestina yameongezeka katika vyuo vikuu vya juu vya Marekani siku ya Jumatatu.
Mahakama ya Juu ya Marekani imepanga kipindi maalum kusikiliza hoja kama Rais wa zamani Donald Trump anaweza kushitakiwa kwa juhudi zake kutaka kuvuruga Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 ambapo alishindwa na Rais Joe Biden.
White House inatathmini njia za kutoa hadhi ya muda ya kisheria na vibali vya kufanya kazi kwa wahamiaji nchini Marekani wanaoishi kinyume cha sheria.
Aharon Haliva ni afisa wa kwanza wa ngazi ya juu Israel kujiuzulu kuhusiana na shambulio la oktoba 7 la hamas dhidi ya Israel.
Masuala mengine pia yatakayojitokeza kati ya nchi hizo mbili ni masuala ya usambazaji maji na usafirishaji wa mafuta na gesi
Sunak alisema serikali imekodisha ndege za kibiashara na imewapatia mafunzo wafanyakazi ili kuwapeleka wahamiaji nchini Rwanda
Jina la MK lina upinzani linafanana na tawi la silaha la ANC ambalo Mandela aliliongoza enzi za ubaguzi wa rangi.
Kampuni ya Tiktok siku ya Jumapili ilitoa wasi wasi wake juu ya masuala ya uhuru wa kujieleza kuhusiana na muswaada uliopitishwa na baraza la wawakilishi wa Marekani ambao unataka kuupiga marufuku
Hoja za ufunguzi zinatarajiwa kuanza Jumatatu katika kesi ya New York inayomkabili Donald Trump, kesi ya kwanza ya jinai kuwahi kuwasilishwa dhidi ya rais wa zamani wa Marekani.
Pandisha zaidi