Svoboda | Graniru | BBC Russia | Golosameriki | Facebook

Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 29, 2024 Local time: 11:00

'Jimbo letu liko katika Mshtuko,' - Gavana wa Maryland


Gavana Wes Moore
Gavana Wes Moore

Gavana wa Jimbo la Maryland, Wes Moore, ameweka wazi kuwa hapakuwa na kitendo chochote cha kigaidi baada ya daraja kuu katika mji wa Baltimore kubomoka Jumanne asubuhi wakati meli iliyobeba mizigo kugonga nguzo yake.

Moore alisema uchunguzi wa awali ulionyesha ni tukio la “ajali” na hapakuwa na “ushahidi wa kutegemewa kuwepo shambulizi la kigaidi.” Aliahidi kutoa fedha na kuwashukuru waokoaji kwa moyo wao.

Daraja la Maryland lililobomoka.
Daraja la Maryland lililobomoka.

Magari kadhaa yalianguka katika maji baridi mapema Jumanne, na waokoaji wanawatafuta manusura wa ajali hiyo.

Waendeshaji wa mali hiyo ya mizigo walipoteza nishati ya umeme na kutoa tahadhari kabla ya chombo hicho kugonga katika daraja la Francis Key Scott, na kuiwezesha mamlaka ya usafiri kudhibiti idadi ya magari yaliyokuwa yanapita wakati huo katika daraja, Moore alisema.

Watu wawili waliokolewa, na haikuwa bayana wengine wangapi inawezekana wako ndani ya maji.

Chanzo cha habari hii ni kituo cha televisheni cha WJLA

Forum

XS
SM
MD
LG