Svoboda | Graniru | BBC Russia | Golosameriki | Facebook

Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 27, 2024 Local time: 20:38

Ghasia za magenge zimeua zaidi ya watu 1,500 huko Haiti; Inasema UN


Ghasia za magenge zinazoendelea huko Haiti ambazo pia zimesababisha maafa kwa jamii.
Ghasia za magenge zinazoendelea huko Haiti ambazo pia zimesababisha maafa kwa jamii.

UN inasema vita vya magenge vimeongezeka wakati wapinzani wenye silaha wakijihusisha na wimbi jipya la mashambulizi

Ghasia za magenge zimeua zaidi ya watu 1,500 nchini Haiti hadi sasa mwaka huu, Umoja wa Mataifa umesema Alhamisi wakati ikilaani kuendelea kwa silaha zinazomiminika katika taifa hilo la kisiwa cha Caribbean.

Umoja wa Mataifa umeielezea hali hiyo kama kichocheo katika nchi hiyo iliyokumbwa na machafuko. “Inashangaza kwamba licha ya hali ya kutisha katika ardhi, silaha bado zinaendelea kumiminika,” Volker Türk, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, alisema katika taarifa.

“Ninatoa wito wa utekelezwaji mzuri zaidi katika vikwazo vya silaha. Umoja wa Mataifa umesema watu kadhaa wamekumbwa na kile kinachoitwa madaraja ya kujilinda mwaka huu. Wengi wa wanachama wa magenge hayo ni wahalifu waliohukumiwa, 4,000 kati yao wametoroka kutoka magereza mawili makubwa nchini Haiti. Vitendo hivi vyote ni vya kuchukiza na lazima visitishwe mara moja,” Türk alisema.

Umoja wa Mataifa umesema vita vya magenge vimeongezeka katika wiki za hivi karibuni wakati wapinzani wenye silaha nzito wakijihusisha na wimbi jipya la mashambulizi, ikijumuisha uvamizi katika vituo vya polisi na uwanja wa ndege wa kimataifa.

Forum

XS
SM
MD
LG