Svoboda | Graniru | BBC Russia | Golosameriki | Facebook

Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 29, 2024 Local time: 02:25

Rais Ruto awalaumu maafisa wa serikali kwa uzembe kufuatia mlipuko mbaya wa gesi


Watu wakikimbilia kwenye usalama kufuatia mlipuko wa gesi katika eneo la Embakasi Nairobi Februari 2, 2024 Picha na LUIS TATO / AFP.
Watu wakikimbilia kwenye usalama kufuatia mlipuko wa gesi katika eneo la Embakasi Nairobi Februari 2, 2024 Picha na LUIS TATO / AFP.

Rais wa Kenya William Ruto Jumamosi amewalaumu maafisa wa serikali kwa uzembe na rushwa kufuatia mlipuko mbaya wa gesi uliotokea jijini Nairobi na kuua watu watatu na kujeruhi wengine 280.

Lori lililokuwa limebeba mitungi ya gesi lilipuka kabla ya saa sita usiku siku ya Alhamisi huko Embakasi, wilaya moja katika mji mkuu wa Nairobi yenye wakazi wengi, na kusababisha uharibifu mkubwa na kupelekea watu kukimbia ili kunusuru maisha yao.

Taasisi ya Petroli ya Afrika Mashariki ilisema Ijumaa kwamba mlipuko huo ulitokea kwenye ghala haramu ya kujazia na kuhifadhi mafuta, ambako mmliki wake na baadhi ya wateja walikutwa na hatia na kuhukumiwa mwezi Mei mwaka 2023.

Lakini Mamlaka ya Mazingira Kenya (NEMA) imesema Jumamosi kwamba kampuni ya nishati Maxxis Nairobi Energy ilipata leseni tarehe 2 Februari mwaka jana kusimamia ghala hiyo.

“Uchunguzi wa awali umebaini kuwa maafisa wanne wa NEMA walitoa leseni bila kuheshimu taratibu na kwa hiyo wana hatia,” mwenyekiti wa bodi ya NEMA Emilio Mugo amesema katika taarifa.

Forum

XS
SM
MD
LG