Svoboda | Graniru | BBC Russia | Golosameriki | Facebook

Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 27, 2024 Local time: 09:28

Shambulizi la nadra Afghanistan lauwa watu 3


Shambulizi la nadra la kujitoa muhanga katika mji wa kusini nchini Afghanistan, ambako inajulikana kuna  makao mkuu ya Taliban, limeuwa takriban watu watatu, na kujeruhi zaidi ya dazeni mapema Alhamisi.

Serekali ya Taliban, imesema waathirika walikuwa wamekusanyika nje ya benki inayoendeshwa rasmi ya New Kabul, kupokea mishahara yao wakati mjitoa muhanga alipotegua vilipuzi alivyovifunga mwilini mwake.

Walioshuhudia na maafisa wa eneo wameripoti kwamba walio jeruhiwa walipelekwa kwenye hospitali ya eneo hilo wengine wakiwa wamepata majeraha mabaya.

Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya Taliban, katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, amesema shambulizi hilo linafanyiwa uchunguzi. Hakuna kundi ambalo limetangaza kuhusika na shambulizi hilo baya.

Forum

XS
SM
MD
LG