Kamishna mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia maswala ya haki za binadamu, Volker Turk amezitembelea kambi za watu waliokoseshwa makazi kaskazini mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Pentagon imesema Lloyd Austin na Admirali Dong Jun wa China walijadili uhusiano wa ulinzi na masuala ya usalama wa kimataifa
Boti ilikuwa imebeba jumla ya watu 12 wengi wao wakiwa wakulima msimamizi wa wilaya ya Caia aliliambia shirika la habari la AFP.
Waziri wa mambo ya nje wa Israel amesema amewasiliana na mataifa zaidi ya 30 kushinikiza vikwazo dhidi ya mpango wa makombora wa Iran.
Mvua ilianza usiku kucha na kuvuruga safari za ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dubai
Kundi la mataifa yanayozalisha mafuta la OPEC+, baada ya kupoteza uanachama wa Angola miongoni mwa wengine katika miaka ya karibuni sasa linalenga kuikaribisha Namibia kujiunga nalo
Idara ya kupambana na ufisadi nchini Nigeria imesema kuwa tayari imepata karibu dola milioni 27 kufuatia uchunguzi dhidi ya waziri wa serikali aliyesimamishwa kazi, pamoja na maafisa wengine.
Raia kati ya 10 na 15 wameuwawa katika mashambulizi ya wikendi eneo la Beni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ikiwa ni mashambulizi mapya yanayoaminiwa kutekelezwa na kundi la ADF linaloshirikiana na Islamic State, vyanzo vya ndani vimeeleza Jumapili.
Umoja wa Ulaya umesema Ijumaa kuwa utaipatia Misri dola bilioni 1.7 kama msaada wa muda mfupi ili kuisaidia nchi hiyo kujenga uchumi wake.
Wafanyakazi wa misaada nchini Sudan wamesema kwamba mapigano ya mwaka mmoja nchini humo yamesababisha mamilioni ya watu kukoseshwa makazi na kukabiliwa na njaa.
Polisi nchini Ethiopia wamewakamata washukiwa 13 juu ya mauwaji ya kiongozi maarufu wa upinzani kutoka jimbo la Oromia, chombo cha habari cha ndani kimesema.
Pandisha zaidi