Jeshi la Kenya lilifanya operesheni Alhamisi kuwaokoa wahanga wa mvua kubwa iliyosababisha vifo vya darzeni za watu kote Afrika Mashariki katika muda wa mwezi mmoja uliopita.
Wabunge wanane wa Uganda wako Nairobi Kenya kwa ziara ya mafunzo juu ya kushughulikia changamoto za ukuaji wa miji nchini humo ikiwemo udhibiti makazi duni na kupitisha sera mahiri za ukuaji wa miji mikubwa.
Jumla ya watu 118 walikuwa waathirika wa mauaji holela yaliyotekelezwa na polisi wa Kenya mwaka uliopita, makundi ya haki za binadamu ya ndani na ya kimataifa yamesema katika ripoti iliyochapishwa Jumatano, yakilaani “kutowajibishwa” kwa maafisa wa usalama waliohusika katika mauaji hayo.
Kenya imetoa tahadhari ya mafuriko wakati mvua kubwa zikinyesha katika eneo hilo. Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya limesema mafuriko katika taifa hilo la Afrika Mashariki yameua watu 38 na zaidi ya 11,000 wamekoseshwa makazi.
Wakulima nchini Kenya waliopewa mbolea ghushi watafidiwa na serikali ya Kenya baada ya kampuni moja kutajwa kuwahadaa wakulima na hivyo kuiweka serikali katika hali ngumu kufuatia Sakata hilo.
Madkatari kutoka hospitali za umma nchini Kenya ambao wamekuwa kwenye mgomo wa kitaifa tangu mwezi uliopita, Jumanne wamekusanyika kwenye miji mwili mikubwa, ili kushauriana kuhusu malalamiko yao dhidi ya serikali.
Maafisa wa usalama wa Kenya Jumanne walianza kutoa miili ya waathiriwa kadhaa wa mauwaji yaliyofanywa na dhehebu lililowataka waumini wao wajiuwe kwa kukaa na njaa ili kwenda kukutana na Yesu
Wanamgambo wa Kiislamu wa kundi la al-Shabab Alhamisi walishambulia hoteli maarufu karibu na ikulu ya rais katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, vyanzo vya usalama na mashahidi walisema.
Wagonjwa wamekwama katika hospitali mbalimbali nchini Kenya kufuatia mgomo wa madaktari unaolenga kuwezesha utekelezaji wa mahitaji ya nafasi za lazima za mafunzo ya utabibu kwa zaidi ya madaktari waliohitimu 4,000, ajira na mazingira bora ya kazi.
Serikali ya Haiti iliomba rasmi msaada wa usalama kutoka kwa nchi zote kote duniani, zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Wajumbe zaidi ya 350 wa serikali, taasisi za utafiti na makampuni yanayotengeneza mbegu wanakutana Kenya wiki hii kujadili changamoto za upatikanaji wa mbegu –bora kwa ajili ya wakulima wa Kiafrika.
Rais wa Kenya William Ruto amelitaka bunge la Afrika Mashariki kuendelea kuwa kiungo muhimu katika juhudi za kuimarisha ushirikiano na watu wa Afrika Mashariki na mshikamano wa nchi wanachama ili kuboresha maendeleo ya kijamii na kiuchumi ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki.
Pandisha zaidi